Genesis 26:28-31

28Wakamjibu, “Tuliona wazi kuwa Bwana alikuwa pamoja nawe, kwa hiyo tukasema, ‘Inabidi kuwe na kiapo cha mapatano kati yetu, kati yetu na wewe. Na tufanye mkataba pamoja nawe 29kwamba hutatudhuru, kama jinsi nasi hatukuwanyanyasa bali tuliwatendea mema wakati wote na kuwaondoa kwetu kwa amani. Tena sasa umebarikiwa na Bwana.’ ”

30Basi Isaka akawaandalia karamu, nao wakala na kunywa. 31Kesho yake asubuhi na mapema, wakaapizana wao kwa wao. Kisha Isaka akawaruhusu waende zao, wakamwacha Isaka kwa amani.

Copyright information for SwhKC